MUNGU WA MAAGANO
Yer
33:19-22 SUV
*Neno la BWANA likamjia Yeremia,
kusema, BWANA asema hivi, Kama mkiweza kulivunja agano langu la mchana, na
agano langu la usiku, hata usiwepo tena mchana na usiku kwa wakati wake, ndipo
agano langu nililolifanya na Daudi, mtumishi wangu, laweza kuvunjika, hata
asiwe na mwana wa kumiliki katika kiti chake cha enzi; tena agano langu
nililofanya na Walawi makuhani, wahudumu wangu, laweza kuvunjika. Kama vile
jeshi la mbinguni haliwezi kuhesabiwa, wala mchanga wa bahari kupimwa; ndivyo
nitakavyoongeza wazao wa Daudi, mtumishi wangu, na Walawi wanaonihudumia*
Dan 9:4
*Nikamwomba BWANA, Mungu wangu,
nikaungama, nikasema, Ee Bwana, Mungu mkuu, mwenye kutisha, ashikaye maagano na
rehema kwao wampendao, na kuzishika amri zake*
*Watu wengi wanashindwa kutembea na
Mungu kwa muda mrefu kwa sababu hawajamwelewa mungu namna anavyo fanya kazi
zake,na moja kati ya vipengere vya muhimu katika kutembea na Mungu katika
Maisha ni kutembea na Mungu kiagano*
Hakuna jambo litakalo kupa uhakika wa
Maisha yako ya sasa na ya baadae kama kuwa na agano na Mungu hii ni Muhimu sana
Tunaposoma neno la mungu katika
waebrania 11,tunawaona mashujaa wa Imani wakitajwa,lakini utaona asilimia 99 ya
hawa wanaoitwa mashujaa wa imani ushujaa wao ulitokana na kutembea na mungu
kiagano.
Ni ukweli usiopingika ya kuwa zipo
ahadi nyingi zinazogusa kila kona ya Maisha ya mtu katika Biblia,Mungu ameahidi
uponya,ulinzi,uzao,mafanikio,msaada wa haraka n.k ,lakini si watu wengi
wanazifikia ahadi hizo,unaweza ukazijua ahadi zote za Mungu lakini utimilifu
wake ni matokeo ya Agano.
Mungu si Mungu wa Ahadi ni Mungu wa
Maagano,yeye Hushika maagano na Rehema
Dan 9:4
*Nikamwomba BWANA, Mungu wangu,
nikaungama, nikasema, Ee Bwana, Mungu mkuu, mwenye kutisha, ashikaye maagano na
rehema kwao wampendao, na kuzishika amri zake*
Hii ndio siri iliyofichwa tangu zamani
za kale,ni hekima iliyofichwa na ni maajabu ya ufalme yanayoleta uhakika wa
Maisha ya sasa nay a Baadae.
Agano na Mungu ni nini?
Agano na Mungu ni makubaliano yako
wewe na Mungu yanayo Ma Mungu uhalali wa kukusaidia katika maeneo Fulani ya
kimaisha,ni Mkataba kati ya pande mbili unaohusisha utekelezaji wa majukumu kwa
faida ya wote,maana yake Mungu atakupa faida na wewe ni lazima ufanye jambo la faida
kwake,ni makubaliano ya kutembea Pamoja katika eneo Fulani.
Amo 3:3
*Je! Watu wawili waweza kutembea
pamoja, wasipokuwa wamepatana*?
Hebu tuangalie mfano wa agano la Mung
una Ibrahimu
Mwa
17:1-25 SUV
*Abramu alipokuwa mtu wa miaka tisini
na kenda, BWANA akamtokea Abramu, akamwambia, Mimi ni Mungu Mwenyezi, uende
mbele yangu, ukawe mkamilifu. Nami nitafanya agano langu kati ya mimi na wewe,
nami nitakuzidisha sana sana. Abramu akaanguka kifudifudi. Mungu akamwambia,
akasema, Mimi, agano langu nimefanya nawe, nawe utakuwa baba wa mataifa mengi,
wala jina lako hutaitwa tena Abramu, lakini jina lako litakuwa Ibrahimu, kwani
nimekuweka uwe baba wa mataifa mengi. Nitakufanya uwe na uzao mwingi sana, nami
nitakufanya kuwa mataifa, na wafalme watatoka kwako. Agano langu nitalifanya
imara kati ya mimi na wewe, na uzao wako baada yako, na vizazi vyao, kuwa agano
la milele, kwamba nitakuwa Mungu kwako na kwa uzao wako baada yako. Nami
nitakupa wewe na uzao wako baada yako nchi hii unayoikaa ugeni, nchi yote ya
Kanaani, kuwa milki ya milele; nami nitakuwa Mungu wao. Mungu akamwambia
Ibrahimu, Nawe ulishike agano langu, wewe na uzao wako kwa vizazi vyao baada
yako. Hili ndilo agano langu utakalolishika, kati ya mimi na wewe, na uzao wako
baada yako, Kila mwanamume wa kwenu atatahiriwa. Mtatahiriwa nyama ya magovi
yenu, na jambo hilo litakuwa ishara ya agano kati ya mimi na ninyi. Mtoto wa
siku nane atatahiriwa kwenu, kila mwanamume katika vizazi vyenu, mzaliwa
nyumbani, na mnunuliwa kwa fedha, kila mgeni asiyekuwa wa uzao wako. Mzaliwa
nyumbani mwako, na mnunuliwa kwa fedha yako, lazima atahiriwe; na agano langu
litakuwa katika mwili wenu, kuwa agano la milele. Na mwanamume mwenye govi
asiyetahiriwa nyama ya govi lake, mtu yule atatengwa na watu wake; amelivunja
agano langu. Mungu akamwambia Ibrahimu, Sarai mkeo, hutamwita jina lake Sarai,
kwa kuwa jina lake litakuwa Sara. Nami nitambariki, na tena nitakupa mwana
kwake, naam, nitambariki, naye atakuwa mama wa mataifa, na wafalme wa kabila za
watu watatoka kwake. Ndipo Ibrahimu akaanguka kifudifudi akacheka, akasema
moyoni, Je! Mtu wa umri wa miaka mia, kwake atazaliwa mtoto? Naye Sara mwenye
umri wa miaka tisini atazaa? Ibrahimu akamwambia Mungu, Lau kwamba Ishmaeli
angeishi mbele yako. Mungu akasema, Sivyo, lakini Sara mkeo atakuzalia mwana wa
kiume, nawe utamwita jina lake Isaka. Nami nitafanya agano langu imara kwake
kuwa agano la milele kwa ajili ya uzao wake baada yake. Na kwa habari za
Ishmaeli nimekusikia, nimembariki, nitamzidisha, nami nitamwongeza sana sana*
Katika mfano huu wa andiko hapo juu
utaona Kuna vipengere vinne ambavyo vinakamilisha agano
1. *Mungu ndiye anayekupa agano*
Tofauti na watu wengi wanavyofahamu ya
kuwa ni wao wanaweka agano na Mungu,kibiblia ni Mungu ndiye anayekuba agano,na
Mungu akikupa agano agano lake ni la Milele.
Mungu alishamaliza kuandika maagano
yaani vipengere vya makubaliano katika maeneo mbalimbali na nini atakachofanya
utakapokubali kuingia nae agano,vipengere hivi ndio tunaviita ahadi,hii ndio
sababu haiwezi kukusaidia sana wewe kushika vipengere vya agano kabla ya
kuingia agano na Mungu
Mwa
17:1-25 SUV
*Abramu alipokuwa mtu wa miaka tisini
na kenda, BWANA akamtokea Abramu, akamwambia, Mimi ni Mungu Mwenyezi, uende
mbele yangu, ukawe mkamilifu. Nami nitafanya agano langu kati ya mimi na wewe,
nami nitakuzidisha sana sana*
Unapoona kuna haja ya kutembea na
Mungu katika eneo Fulani la kimaisha,anagalia vipengere vya neno la Mungu
vinavyozungumzia changamoto unayoipitia kisha ingia katika agano na Mungu
2. *Mungu anakubadilisha jina na kukupa
utambulisho wako halisi*
Mara nyingi majina yetu ndiyo
yanayotutambulisha kwa watu,ni majina tumepewa na wazazi wetu,lakini lipo jina
linalobeba utambulisho wako halisi na jina hilo ni jina la kiagano,ni jina
ambalo Mbingu inakutambua nalo.
Unapotembea na Mungu kiagano hauwezi
kubabe utambulisho ule ule ambao ulikuwa nao kabla ya agano hii ni kwa sababu
jina la Mtu hubeba Nguvu zake,mipaka yake na uwezo wake,pia hubeba utambulisho
wake na tabia zake
Hii ndio sababu Mungu akitaka kutembea
na wewe atakupa utambulisho mpya ambao utaendana na agano analokupa,hii
inamaana kuwa atakupa nguvu mpya,akili mpya ,tabia mpya n.k
Mwanzo 17
* Mungu
akamwambia, akasema, Mimi, agano langu nimefanya nawe, nawe utakuwa baba wa
mataifa mengi, wala jina lako hutaitwa tena Abramu, lakini jina lako litakuwa
Ibrahimu, kwani nimekuweka uwe baba wa mataifa mengi*
Si ibrahimu peke yake ambaye
alibadilishwa jina,ipo mifano ya mashujaa wengine pia,unasoma
Mwa 32:28
*Akamwambia, Jina
lako hutaitwa tena Yakobo, ila Israeli, maana umeshindana na Mungu, na watu,
nawe umeshinda*
Yn 1:42 SUV
*Akampeleka kwa
Yesu. Naye Yesu akamtazama, akasema, Wewe u Simoni, mwana wa Yohana; nawe
utaitwa Kefa *(tafsiri yake Petro, au Jiwe).
Japokuwa si wote ambao Mungu huwapa
agano hubadilishwa majina,lakini hii huwa ni hatua muhimu sana kuelekea
mabadiliko katika kiwango cha kiagano.
3. *Ahadi za Agano*
Ahadi za agano ni matokeo ya uaminifu
wako kwa Mungu juu ya vipengere vya kiagano,kwa lugha rahisi tunaweza sema
faida za kuingia agano na Mungu.
Mwanzo 17
“…Nami nitakupa
wewe na uzao wako baada yako nchi hii unayoikaa ugeni, nchi yote ya Kanaani,
kuwa milki ya milele; nami nitakuwa Mungu wao. Mungu akamwambia Ibrahimu, Nawe
ulishike agano langu, wewe na uzao wako kwa vizazi vyao baada yako. Hili ndilo
agano langu utakalolishika, kati ya mimi na wewe, na uzao wako baada yako, Kila
mwanamume wa kwenu atatahiriwa…”
unapoamua kujitoa kwa uaminifu juu ya
agano lako na Mungu ndipo Mungu atakutimizia ahadi zake za kiagano.
4. *Majukumu ya kiagano*
Hapa ndio wengi huwa tunafeli,wengi
hutelekeza majukumu katika nyakati za kwanza na baada ya muda hujisahau au
kuacha kabisa.
Hii ndio sababu mwanadamu hawezi
kubaki wa kuaminiwa katika eneo la maagano,ni Mungu peke yake hubaki wa kuaminiwa
Malaki
3:6 SRUV
*Kwa kuwa mimi, BWANA, sina kigeugeu;
ndio maana ninyi hamkuangamizwa, enyi wana wa Yakobo*
Ni Gharama katika kutekeleza majukumu
ya kiagano,na wakati mwingine unaweza usipende kile ambacho Mungu anakwambia
ufanye lakini kama unataka kufurahia mabadiliko ni lazima ufanye.
Wakati nimeingia kwenye agano na Mungu
la utumishi kuna mamboa ambayo niliambiwa sitakiwi kufanya,mambo hayo si dhambi
kwa mtu wa kawaida kufanya lakini kwangu ni mwiko.
Ibrahimu aliambiwa mambo yafuatayo.
i.
Mimi ni Mungu
Mwenyezi, uende mbele yangu, ukawe mkamilifu.
ii.
Hili ndilo agano
langu utakalolishika, kati ya mimi na wewe, na uzao wako baada yako, Kila
mwanamume wa kwenu atatahiriwa. Mtatahiriwa nyama ya magovi yenu, na jambo hilo
litakuwa ishara ya agano kati ya mimi na ninyi. Mtoto wa siku nane atatahiriwa
kwenu, kila mwanamume katika vizazi vyenu, mzaliwa nyumbani, na mnunuliwa kwa
fedha, kila mgeni asiyekuwa wa uzao wako. Mzaliwa nyumbani mwako, na mnunuliwa
kwa fedha yako, lazima atahiriwe; na agano langu litakuwa katika mwili wenu,
kuwa agano la milele.
Hasara
za kutokushika makubaliano.
i.
Kutengwa mbali na
watu wako
……
Na mwanamume mwenye govi asiyetahiriwa nyama ya govi lake, mtu yule atatengwa
na watu wake; amelivunja agano langu….
ii.
Kuharibiwa kwa
kazi za mikono yako
Muh 5:6
Usikiache kinywa chako kuukosesha mwili wako;
wala usiseme mbele ya huyo malaika ya kwamba umepitiliwa; kwani Mungu
akukasirikie sauti yako, na kuiharibu kazi ya mikono yako?
iii.
Kutokufika kule
ambako Mungu alitaka ufike
Hes 20:12 SUV
*BWANA akamwambia Musa na Haruni, Kwa kuwa
hamkuniamini mimi, ili kunistahi mbele ya macho ya wana wa Israeli, basi kwa
sababu hiyo, hamtawaingiza kusanyiko hili katika ile nchi niliyowapa*
*Faida za Kuwa na Agano Na Mungu*
i.
Kuwa na uhakika
wa Baadae yako
ii.
Kutembea na mungu
katika eneo ambalo umeweka nae agano,kama ni katika Biashara,kazi au ndoa
iii.
Agano linakupa
Ulinzi wa Kiungu kwenye eneo la kiagano
iv.
Agano
linahakikisha ahadi za Mungu zinatimia sawa sawa na Makubaliano Yenu
v.
Agano linakupa
kibali
vi.
Ni uhakika ya
kuwa Mungu yupo katika eneo lako
NB;
*Unaweza kuingia na Mungu katika agano kutegemeana na uhitaji wa Maisha yako*
Imeandaliwa
na
*Rabbi
and Prophet Calvin Raphason*
Spirit
of life Ministries
Mawasiliano
*0757370010/0797680106/0773700106*

Comments
Post a Comment